Proto na Yasinto (walifariki 257/259) ni kati ya Wakristo wa Misri waliofia imani yao huko Roma, Italia, katika dhuluma ya kaisari Valerian.

Kifodini cha Wat. Proto na Yasinto, mchoro mdogo wa karne ya 14.

Tangu kale wanaheshimiwa na Wakatoliki, Waorthodoksi na Waorthodoksi wa Mashariki kama watakatifu wafiadini.

Papa Damaso I aliwasifu kwa mashairi na kutoa masalia yao ardhini. Karne 15 baadaye vimepatikana tena huko kaburi la Yasinto zima kabisa na mifupa yake imeunguzwa kwa moto kutokana na jinsi alivyouawa [1].

Sikukuu yao huadhimishwa tarehe 11 Septemba[2] au 24 Desemba.

Tazama pia

hariri

Tanbihi

hariri

Viungo vya nje

hariri
  Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.