Nenda kwa yaliyomo

Simoni wa Crepy

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Simoni wa Crepy (au wa Vexin; Bar-sur-Aube, Ufaransa, 1048 hivi - Roma, Italia, 30 Septemba 1082) alikuwa mtawala wa Amiens, Vexin na Valois miaka 1074-1077.

Tangu kale anaheshimiwa kama mtakatifu.

Sikukuu yake inaadhimishwa tarehe 30 Septemba[1].

Baada ya kuoa, alikubaliana na mke wake waachane na mali yao wakatawe monasterini. Hata hivyo, kwa kutoridhika na utajiri wa mazingira ya Condat, baadaye alikwenda kuishi upwekeni kwenye misitu ya Jura.

Kutoka huko aliitwa mara kadhaa kufanya upatanisho kati ya watawala waliopigana vita.

Pia alihiji hadi Nchi takatifu halafu Roma alipofariki huku akisaidiwa sakramenti za mwisho na Papa Gregori VII.

Alizikwa kwenye basilika la Mt. Petro[2].

Tazama pia

[hariri | hariri chanzo]
  • Bury, J. B., The Cambridge Medieval History, Volume III: Germany and the Western Empire, Cambridge University Press, London, 1922, pg. 111
  • Cowdrey, H. E. J., Count Simon of Crepy's Monastic Conversion. The Crusades and Latin Monasticism, 11th–12th Centuries, Ashgate Publishing, Brookfield, VT, 1999
  • Herbert Thurston e Donald Attwater (cur.), Butler's Lives of the Saints: September, pp. 283-284, The liturgical press, Collegeville 2000. ISBN 0-8146-2385-9.

Viungo vya nje

[hariri | hariri chanzo]
  • Ferroul-Montgaillard, Histoire de l'abbaye de St-Claude, ed. F. Gauthier, 1834 [1]
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.