Nenda kwa yaliyomo

Dhambi ya mauti

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mkristo akiungama dhambi zake huko Lviv, Ukraine.

Dhambi ya mauti ni dhambi kubwa ambayo inaua uzima wa kiroho kadiri ya maadili ya Kanisa Katoliki[1] na baadhi ya madhehebu mengine ya Ukristo[2].

Msingi katika Biblia

[hariri | hariri chanzo]

Istilahi hiyo inapatikana kwanza katika 1Yoh 5:16-17 kwa kutofautisha uzito wa dhambi. Kabla yake, Yesu mwenyewe alikuwa ameonyesha uwepo wa tofauti ya namna hiyo (Mk 3:28-29).

Kwenye Agano la Kale pia adhabu za dhambi zinatofautiana kadiri ya uzito wake: kwa mfano, kadiri ya Torati, uuaji wa mtu au kutoa unabii wa uongo au kuzini si sawa na kuua punda wa mtu, bali ni makosa yanayodai mtendaji auawe.

Maelezo ya Kanisa Katoliki

[hariri | hariri chanzo]

Dhambi kubwa ni kuvunja kwa makusudi amri ya Mungu au ya Kanisa katika jambo kubwa. Hiyo inaitwa dhambi ya mauti kwa kuwa inaua uzima wa Mungu rohoni mwa mtu. (Lk 9:60; 1Kor 11:30; Ef 2:1-5)

Ili dhambi iwe ya mauti yanatakiwa mambo matatu pamoja:

  • jambo lenyewe liwe zito
  • litendwe kwa ujuzi kamili
  • litendwe kwa hiari, yaani ukubali kamili. (Lk 23:34; Mdo 3:17; 13:27; 1Kor 2:8)

Madhara ya dhambi ya mauti ni kujitenga na Utatu Mtakatifu, kupoteza neema ya utakaso, stahili zote na haki ya kuingia mbinguni. Bila kuijuta ni hakika ya kuteseka milele. (Math 7:23; 25:46)

  1. "Catechism of the Catholic Church - PART 3 SECTION 1 CHAPTER 1 ARTICLE 8". www.scborromeo.org. Iliwekwa mnamo 2020-09-28.
  2. "Dictionary : MORTAL SIN". www.catholicculture.org. Iliwekwa mnamo 2023-06-13.
Makala hii kuhusu dini ya Ukristo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Dhambi ya mauti kama historia yake, matokeo au athari zake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.