Nenda kwa yaliyomo

Ubakaji

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Ubakaji wa Lukresya, uliomfanya ajiue, ulikuwa kati ya sababu za mfululizo wa matukio yaliyokomesha Ufalme wa Roma na kuanzisha Jamhuri ya Roma mwishoni mwa karne ya 6 KK.
Maandamano huko Bangalore, India, yakidai haki kwa mwanafunzi aliyebakwa huko Delhi mwaka 2012. Ubakaji nchini huko unaongezeka kwa kasi kutokana na dharau kwa wanawake.

Ubakaji (kutoka mzizi wa Kiarabu) ni tendo la kumlazimisha mtu afanyiwe asichokubali. Mara nyingi neno hili linatumika kuhusu ngono isiyo ya hiari upande mmojawapo.

Ingawa kwa kawaida unafanyika dhidi ya wanawake, unatokea pia dhidi ya wanaume, mbali ya watoto na walemavu wa akili wasioelewa kinachoendelea[1].

Unaweza kutumia nguvu ya mwili, lakini pia mamlaka, vitisho n.k.

Ni tukio baya kabisa kwa nafsi ya mhanga na pengine kwa afya yake, linaloweza kumuathiri maisha yake yote kama si kusababisha kifo chake, hasa ukifanywa na watu kadhaa pamoja.

Matukio ya namna hiyo yanazidi kutokea hata ndani ya ukoo na mengi hayaripotiwi kwa polisi, yakiwemo yanayotokea magerezani kati ya watu wa jinsia ileile.

Kwa vyovyote, mara nyingi wanaobaka ni watu wanaojulikana sana na mhanga.

Pengine ubakaji hautokani na tamaa, bali ni mpango uliosukwa na viongozi wa nchi au wa jeshi wanaouagiza kwa lengo la kuathiri maadui. Lakini hata vitani, sheria za kimataifa haziruhusu matendo hayo ya kinyama.

Kesi tofauti tena ni ile ya ushirikina unaoagiza k.mf. kubaka mtoto kama njia ya kupona UKIMWI.

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  • Bergen, Raquel Kennedy (1996). Wife rape: understanding the response of survivors and service providers. Thousand Oaks: Sage Publications. ISBN 978-0-8039-7240-7.
  • Denov, Myriam S. (2004). Perspectives on female sex offending: a culture of denial. Aldershot, Hants, England: Ashgate. ISBN 978-0-7546-3565-9.
  • Freedman, Estelle B. (2013). Redefining Rape: Sexual Violence in the Era of Suffrage and Segregation. Cambridge, MA: Harvard University Press.
  • Groth, Nicholas A. (1979). Men Who Rape: The Psychology of the Offender. New York, NY: Plenum Press. uk. 227. ISBN 978-0-7382-0624-0.
  • Pierce, Karen F.; Deacy, Susan; Arafat, K. W. (2002). Rape in antiquity. London: The Classical Press of Wales in association with Duckworth. ISBN 0-7156-3147-0.
  • King, Michael B.; Mezey, Gillian C. (2000). Male victims of sexual assault. Oxford [Oxfordshire]: Oxford University Press. ISBN 978-0-19-262932-6.
  • Lee, Ellis (1989). Theories of Rape: Inquiries Into the Causes of Rape. Taylor & Francis. uk. 185. ISBN 978-0-89116-172-1.
  • Marnie E. Rice; Lalumiere, Martin L.; Vernon L. Quinsey (2005). The Causes of Rape: Understanding Individual Differences in Male Propensity for Sexual Aggression (The Law and Public Policy.). American Psychological Association (APA). ISBN 978-1-59147-186-8.
  • McKibbin W.F.; Shackelford T.K.; Goetz A.T.; Starratt V.G. (2008). "Why do men rape? An evolutionary psychological perspective" (PDF). Review of General Psychology. 12: 86–97. doi:10.1037/1089-2680.12.1.86.
  • Palmer, Craig; Thornhill, Randy (2000). A natural history of rape biological bases of sexual coercion. Cambridge, Mass: MIT Press. ISBN 978-0-585-08200-4.
  • Shapcott, David (1988). The Face of the Rapist. Auckland, NZ: Penguin Books. uk. 234. ISBN 978-0-14-009335-3.
  • Smith, Merril D. (2004). Encyclopedia of Rape. Westport, Conn: Greenwood Press. ISBN 978-0-313-32687-5.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii kuhusu mambo ya sheria bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Ubakaji kama historia yake au uhusiano wake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.